HALI YA UFANYAJI MITIHANI KIDATO CHA NNE WILAYANI MAKETE NI SHWARI

Thursday, November 07, 20130 comments

Afisa elimu sekondari wilayani Makete mkoani Njombe Bwana Jacob Meena  amesema kuwa hali ya mitihani ya kidato cha nne inayoendelea kwa sasa  wilayani Makete na Tanzania nzima, kwa upande wa wilaya ya Makete hali ya ufanyaji wa mitihani hiyo haina dosari yoyote hadi hivi  sasa
Akizungumza na kitulo fm inayomilikiwa na halmashauri ya Makete ofisini kwake Bwana Meena amesema kuwa hakuna tatizo lolote lile lililoripotiwa ofisini kwake kuhusu mitihani inayoendelea

Hata hivyo amesema kuwa kuna aina tatu za watahiniwa waliosajiliwa kufanya mitihani hiyo ikiwa ni watahiniwa wa shule(wanafunzi waliokuwepo shuleni kwa kipindi cha miaka minne ),watahiniwa wa kujitegemea na mtihani wa maarifa
Akitoa idadi ya watahiniwa ambao wamesajiliwa kufanya mitihani hiyo wilayani hapa amesema jumla ya wanafunzi ni 1,245 ambapo wanafunzi wa shule ni 1,094 na watahiniwa wa kujitegemea pamoja na maarifa ni 151
Hata hivyo Bw.Meena ametoa wito kwa wanafunzi hao kuwa watumie akili yake ktk ufanyaji wa mitihani hiyo na siyo kutazamia kwa mwenzake kwani akikamatwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake

Na Benson Kyando
Share this article :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. MAKETE BLOG - All Rights Reserved
Designed by Edwin Moshi
Property of Makete District Council