Zoezi
la kufanya ukarabati mkubwa katika chanzo cha maji cha Kidwiva
kilichopo katika kijiji cha Ivalalila wilaya ya Makete mkoa wa Njombe
lililotarajiwa kumalizika leo, limeshindwa kumalizika kama
ilivyotarajiwa
Kauli
hiyo imetolewa na meneja wa mamlaka ya maji makete mjini Bw. Yonas
Ndomba wakati akizungumza na mtandao huu kuhusu maendeleo ya ukarabati
huo ambao umesababisha ongezeko la mgawo wa maji Makete mjini
Meneja
Ndomba amesema walitarajia zoezi hilo likamilike jana au leo Ijumaa
lakini kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kwenye chanzo hicho kwa siku
tatu mfululizo kumepelekea mafundi hao kukwama kuendelea na ukarabati
huo
Amesema
wanatarajia kuendelea na zoezi hilo hapo kesho Jumamosi kama mvua
hazitanyesha wanategemea kumaliza ukarabati huo na hali ya maji kwa
wananchi wa Makete mjini itarejea kama kawaida
Amewaomba wananchi hasa wateja wa maji
kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha matengenezo kwani wanajitahidi
kukamilisha ukarabati huo
Wakati
huo huo Meneja huyo amesema mabomba ya maji kwa ajili ya kuboresha
miundombinu ya maji katika chanzo hicho tayari yamewasili katika kijiji
cha Ivalalila na kinachosubiriwa na ukaguzi wa mabomba hayo kama yana
viwango vinavyotakiwa na serikali
Amesma endapo ukaguzi huo utaonesha kama yana viwango stahili wataendelea na uboreshaji wa miundombinu hiyo
NA EDWIN MOSHI
Post a Comment