WAZAZI WILAYANI MAKETE WATAKIWA KUWABANA WATOTO WAO WENYE MAADILI MABOVU

Thursday, November 07, 20130 comments

Wazazi na walezi wilayani makete Mkoani Njombe wametakiwa kusimamia maadili ya vijana wao na kuhakikisha wanakwenda katika mstaari ulionyooka ili kuondokana na matatizo yanayowapata ambayo pengine yangeweza kuepukika

Hayo yamesemwa na naibu katibu mkuu wa umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Eva Kihwele katika mkutano wa hadhara alioufanya katika kata ya Luwumbu wilayani hapa baada ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata hiyo

Bi Kihwele amesema inashangaza kuona wazazi hasa kina baba wamekuwa mstari wa mbele kuwapiga wake zao kwa madai kuwa wamewakosea lakini wanashindwa kuwaadhibu watoto wao wanaovaa nguo zisizo na maadili ya kitanzania

"Unakuta mtoto wa kike kavaa kimini ama nguo za kubana mpana wewe kama mzazi unaona aibu kumtazama, wa kiume kavaa mlegezo, lakini hamuwakemei na badala yake mnawapiga wake zenu tu kwanini? alisema Kihwele

Amewataka wazazi kuwa mstari wa mbele kuwajenga watoto wao kitabia ili wavae mavazi yenye maadili ya kitanzania ili pamoja na mambo mengine iwe rahisi kwao hata kupata ajira mara baada ya kumaliza masomo yao

Katika hatua nyingine amewataka wazazi kuacha tabia ya kuwaruhusu watoto wao kwenda Dar es Salaam kufanya kazi za ndani kwa madai kuwa ni kuzuri, na badala yake watoto hao huenda kuishi maisha magumu huko na mwishowe wanajiingiza katika vitendo vya kuuza miili yao hivyo kuwaweka katika hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Naibu katibu UWT Taifa yupo wilayani Makete kuendelea na ziara yake ambapo hii leo ametembelea kata za Luwumbu na Ipelele na kutembelea mashamba darasa, mfereji wa umwagiliaji pamoja na ujenzi wa bweni la wanafunzi Ipelele sekondari na kufanya mikutano ya hadhara katika kata hizo
 
Na Edwin Moshi
Share this article :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. MAKETE BLOG - All Rights Reserved
Designed by Edwin Moshi
Property of Makete District Council