WAFANYABIASHARA WALIOBOMOLEWA VIBANDA VYAO MAKETE MJINI WAZIDI KUOMBA VIWANJA

Friday, November 08, 20130 comments

Kutokana na zoezi la bomoa bomoa lililofanyika Makete mjini Wafanyabiashara wamejitokeza kujaza fomu za kuomba viwanja vilivyotangazwa Oktoba 17 mwaka huu na mkurugenzi mtendaji wa halmashuri ya wilaya ya Makete Bwana Iddi Nganya hadi sasa ni watu 28 tu waliomba fomu kwa kibali kutoka katika ofisi ya kata ya Iwawa.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wilayani Makete Bwana Hosea Mpandila amesema kuwa wafanyabiashara walio bomolewa vibanda ni 42 na waliojitokeza kujenga vibanda vipya ni 35 na wafanyabiashara 7 hawajulikani walipokwenda

Pia ameongeza kuwa sehemu ambazo wamesambaza fomu hizo ni pamoja na Kona fomu 6 Mabehewani fomu 58 soko kuu la Makete mjini fomu 60 na Dombwela hawajafuatilia fomu hizo hadi sasa ilikuweza kuzichukua kwa mwenyekiti huyo
Picha na Edwin Moshi, habari kwa hisani ya Kitulo FM
Share this article :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. MAKETE BLOG - All Rights Reserved
Designed by Edwin Moshi
Property of Makete District Council